Waziri Mussa Azan Zungu akishiriki usafi katika fukwe za Salender Bridge
Leo ni siku ua pili ya Wiki ya Machampioni kuelekea Simba Day Agosti 22 mwaka huu itakayofanyika katika Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam, ambapo imeanza jana kwa kuzindua jezi na logo mpya ya klabu. Wiki ya Machampioni itaendelelea kesho kwa dua ya kuwaombea marehemu waliotangulia mbele ya haki ambao ni waasisi wa klabu. Kilele cha shughuli za Wiki ya Machampioni itakua Jumamosi ijayo katika Uwanja wa Benjamin Mkapa.
Wafanyakazi, wanachama na mashabiki wa Simba wakishiriki usafi katika fukwe za Salender Bridge