Habari za Michezo kote Ulimwenguni

Powered by Blogger.
Showing posts with label HABARI. Show all posts
Showing posts with label HABARI. Show all posts

BERNARD MORRISON AACHWA BONGO SIMBA IKIKWEA PIPA




KIUNGO wa Simba, Bernard Morrison ameachwa kwenye msafara wa wachezaji uliokwea pipa leo Desemba 18 kuwafuata wapinzani wao FC Platinum ya Zimbabwe.



Nyota huyo ambaye alisajiliwa kwa mbwembwe akitokea Klabu ya Yanga kwa dili la miaka miwili amekuwa hana nafasi ndani ya Simba inayonolewa na Kocha Mkuu, Sven Vandenbroeck.

Mbali na Morrison nyota mwingine ambaye ameachwa ni Charles Ilanfya ambaye sio chaguo la Sven licha ya uongozi kuweka wazi kwamba usajili wa mchezaji huyo kutoka Klabu ya KMC ilikuwa ni pendekezo la kocha huyo.




Simba imewafuata FC Platinum ikiwa na orodha ya wachezaji 24 ambapo wanatarajiwa kucheza FC Platinum Desemba 23, mchezo wa kwanza kisha ule wa marudiano itakuwa ni kati ya Januari 5-6, Uwanja wa Mkapa.




Nafasi ya Morrison imechukuliwa na kiungo mpya Taddeo Lwanga ambaye ni ingizo jipya akiwa amesaini dili la miaka miwili.

KIKOSI CHA SIMBA KILICHOKWEA PIPA LEO KUWAFUATA WAZIMBABWE

 


KIKOSI cha Simba ambacho kimekwea pipa leo Desemba 18 kuifuata FC Platinum ya Zimbabwe. 


Mchezo huo unatarajiwa kuchezwa Desemba 23 nchini Zimbabwe ni wa Ligi ya Mabingwa Afrika hatua ya kwanza

NYONI: SIMBA ITAIFUNGA FC PLATINUM






KIRAKA wa Klabu ya Simba, Erasto Nyoni amefunguka kuwa anaamini timu hiyo itaibuka na ushindi kwenye mchezo wao wa ugenini dhidi ya Klabu ya FC Platinum unaotarajiwa kupigwa Desemba 23, Harare, Zimbabwe.



Simba tayari imewasili Jijini Harare leo Desemba 18 kwa ajili ya maandalizi ya mwisho ya mchezo huo wa raundi ya kwanza ya michuano ya Klabu Bingwa Afrika.

Simba imefuzu hatua hiyo baada ya kuwaondosha Klabu ya Plateau United ya Nigeria kwenye mchezo wa raundi ya awali.

Akizungumza kuhusu mchezo huo Nyoni amesema: "Tunatumaini utakuwa mchezo mgumu kutokana na ubora wa wapinzani ambao tunakwenda kukutana nao.

"Lakini Wanasimba wanapaswa kutuamini na kuendelea kutuombea kwani tunaenda kwenye mapambano na naamini tunakwenda kushinda mchezo huu,".

SIMBA WATUA KIBABE ZIMBABWE,SERIKALI YAWAPOKEA, MPANDA MPIRA AKOSEKANA




WAWAKILISHI wa Tanzania kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika Klabu ya Simba, leo Desemba 18 wamewasili salama nchini Zimbabwe kwa ajili ya mchezo wa hataua ya kwanza dhidi ya FC Platinum.






Kikiwa chini ya Kocha Mkuu, Sven Vandenbroeck na kocha msaidizi Seleman Matola kimepata bahati ya kuonana na Balozi wa Tanzania nchini Zimbabwe, Profesa Emmanuel Mbennah.




Balozi huyo alipata nafasi ya kupiga picha ya pamoja na viongozi, wachezaji na benchi la ufundi baada ya chakula cha mchana.

Pia amepata nafasi ya kuongea na wachezaji wa timu ya Simba ambao wana kibarua cha kusaka ushindi kwenye mchezo huo unaotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa.




Kikiwa kimeongozana na wachezaji 24 wanaoongozwa na nahodha John Bocco pamoja na Mohamed Hussein, 'Tshabalala' atakosekana mpanda mpira Bernard Morrison na Charlse Ilanfya ambao hawapo kwenye mpango wa Sven.

Simba SC yaisogelea Yanga juu



Simba imeendeleza moto wa kula viporo vyake baada ya jana kuwachapa wenyeji wao Mbeya City kwa bao 1-0, shukrani kwa kazi ya kiume ya mshambuliaji John Bocco aliyeitoa kibabe timu yake.

Hata hivyo haikuwa rahisi kwa Simba kupata ushindi huo baada ya wenyeji kuonyesha tofauti kubwa wakicheza soka la pasi na kasi lakini shida yao ikaja katika kumalizia wakikutana na ukuta mgumu wa wekundu hao chini ya mkongwe Joash Onyango na Ibrahim Ame ambaye jana alipata nafasi nyingine ya kuanza katika kikosi cha kwanza.

Simba ndiyo walikuwa wa kwanza kufanya shambulizi kali dakika ya 20 na krosi ya Clatous Chama almanusura iitangulize timu yake, Bocco akishindwa kuunganisha na mpira kugonga mwamba na kipa Lameck Kanyonga kuuwahi.

Muda mrefu wa mchezo huo timu zote zilionekana kushindana kwa soka la katikati ya kiwanja wakishindwa kufika vyema katika kumalizia kufunga.


Ukuta wa Simba ulilazimika kufanya kazi ya ziada kupambana na mshambuliaji mwenye wa na Onyango.ADVERTISEMENT


Bocco dakika ya 33 akabadili ubao wa mabao akifunga bao safi la ufundi akipokea mpira kwa mguu wa kushoto kisha kumtoka kwa akili beki Juma Shemvuni na kufunga kwa shuti la ufundi akitumia mguu wa kulia akipokea pasi ya Chama.

Bao hilo lilikuwa ni la nane kwa msimu huu kwa Bocco akiendelea kufufua matumaini ya kuchukua tena kiatu cha ufungaji bora msimu huu huku bao hilo pia likiwa la 32 kwa timu yake.

Kuingia kwa bao hilo kuliwaamsha wenyeji na kuanza kujipanga tena kwa utulivu ambapo dakika 35 Seleman Ibrahim almanusura afunge bao kwa kichwa akipokea krosi kali ya Mpoki Mwakinyuke iliyowapita mabeki wa Simba na kukutana nayo nyuma yao.

Simba waliendelea kuliandama lango la Mbeya City ambapo dakika ya 37, Keneth Kunambi alifanya kazi nzuri kumbana Bocco aliyekuwa anasubiri kupiga bao la pili akiokoa krosi nzuri ya beki wa kulia Shomari Kapombe.

Simba ilipata nafasi nzuri katika kumaliza dakika 45 za kwanza lakini Meddie Kagere alishindwa kumalizia kwa kishwa krosi ya Hassan Dilunga.

Bao hilo lilidumu hadi dakika 45 za kwanza zinamalizika kwa Simba kutoka kifua mbele dhidi ya Mbeya City katika Uwanja wa Sokoine Mkoani Mbeya.

Kipindi cha pili Simba waliingia kwa mabadiliko wakimtoa Bocco nafasi yake ikichukuliwa Chriss Mugalu akirejea baada ya kukaa nje kwa muda mrefu akiwa majeruhi.

Licha ya kuwa na mabadiliko hayo katika kikosi cha mabingwa hao watetezi wa Ligi Kuu, hakukuwa na mabadiliko yoyote kwa upande wa mabao.

Wekundu wa Msimbazi sasa wamefikisha pointi 29, wakiishusha Azam FC katika nafasi ya pili ya msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.




Mkutano mdogo Simba waja

Kamati ya Uchaguzi ya Simba imesisitiza kuwa, rais mpya wa klabu hiyo atakayechaguliwa kwenye uchaguzi mdogo atakuwa chaguo la wana Simba na si vinginevyo.


Simba itafaya uchaguzi mdogo Februari 7 ili kuziba nafasi ya mwenyekiti, Swedi Mkwabi aliyejiuzulu mwaka jana.

Mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi huo, Boniface Lihamwike alisema hakutokuwa na mchezo katika mchakato huo, akisisitiza kuwa utakuwa huru na wa haki.

“Atakayechaguliwa atachaguliwa kwa haki na wanachama wa Simba watampata kiongozi chaguo lao,” alisisitiza.

Moja ya sifa kubwa za mgombea wa nafasi hiyo, mbali ya kuwa Mtanzania, pia anapaswa kuwa mwanachama wa Simba kwa kipindi kisichopungua miaka mitatu na mwenye elimu ya shahada ya kwanza inayotambuliwa na TCU na kila mgombea atalipia Sh300,000 ya fomu zinazoanza kutolewa leo hadi Desemba 24

Desemba 27 na 28 ni usaili, kutakuwa na siku nne za mapingamizi kuanzia Desemba 29 na Januari 5 hadi Februari 6 kitakuwa ni kipindi cha kampeni kwa wagombea wote waliopitishwa.

Alisema uchaguzi huo utaendeshwa chini ya kanuni za uchaguzi za Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kwa kuwa katiba ya Simba inawaruhusu kufanya hivyo kwa kuwa klabu hiyo haina kanuni za uchaguzi.

Simba ni Chama, Bocco tu






Kasi ambayo Yanga inaenda nayo kwenye Ligi Kuu Bara msimu huu ni kama inawavuruga mabingwa watetezi wa ligi hiyo Simba, ambao juzi walipata ushindi kiduchu wa bao 1-0 dhidi ya Mbeya City.

Licha ya Mbeya City kuwa ya tatu kutoka chini ya misamo wa ligi, iliibana Simba katika mchezo huo na kama ingeongeza kasi kidogo mchezo ungemalizika kwa sare.


Simba inacheza mechi zake katika presha ya kutetea ubingwa wao na kusaka taji la nne mfululizo la ubingwa msimu huu, huku kasi ya wapinzani wao wakubwa, Yanga ambayo imeanza kufunga idadi kubwa ya mabao katika mechi zake ikizidi kuwachanganya.

Miamba hiyo imezidiwa na Yanga pointi nane, huku pia ikiwa na mechi mbili mkononi za viporo dhidi ya KMC wanayocheza nayo Jumatano na dhidi ya Dodoma Jiji ugenini.

Ukiondoa mechi hizo, Simba ina mechi nne, mbili za kumaliza mzunguko wa kwanza wa ligi dhidi ya Namungo iliyopangwa kufanyika Jumapili na dhidi ya Azam itakayofanyika Desemba 27, wakati watani zao, Yanga wakiwa na michezo miwili dhidi ya Dodoma Jiji (Desemba 19) na itamaliza mzunguko wa kwanza kwa kucheza na Ihefu ugenini Desemba 26

SIMBA KAZINI LEO KUSAKA POINTI TATU MUHIMU DHIDI YA KMC




BAADA ya kumaliza kazi ya kusaka pointi tatu mbele ya Mbeya City, Uwanja wa Sokoine Mbeya kwa kushinda bao 1-0 Leo ina kazi ya kusaka pointi nyingine mbele ya KMC.






Tayari kikosi cha Simba kinachonolewa na Kocha Mkuu, Sven Vandenbroeck kimeshatia timu Dar es Salaam, jana Desemba 14 kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wao ujao wa Ligi Kuu Bara.




Mchezo huo unatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa kutokana na timu zote kuwa na mwendo mzuri ndani ya uwanja zikiwa kwenye viwanja vya Dar.

KMC imetoka kupoteza kwa kufungwa bao 1-0 dhidi ya Mtibwa Sugar Uwanja wa Jamhuri, Morogoro itaingia ndani ya uwanja ikiwa na hasira za kulipa kisasi cha kupoteza.




Ofisa Habari wa KMC, Christina Mwagala amesema kuwa wapo tayari kwa mchezo huo na wanahitaji pointi tatu muhimu.




Vandenbroeck, Kocha Mkuu wa Simba amesema kuwa anaamini utakuwa mchezo mgumu ila anahitaji pointi tatu muhimu.

TANO BORA YA WAFUNGAJI BONGO









LIGI Kuu Bara msimu wa 2020/21 imezidi kuchanja mbunga huku vita kila seheu ikiwa ni ya moto kwa timu na mchezaji mmoja ndani ya timu.




Vita ya ufungaji nayo pia inazidi kupamba moto ambapo kwa msimu uliopita kiatu kilisepa na kuibukia Simba kwa mshambuliaji, Meddie Kagere ambaye alifunga jumla ya mabao 22.

Kwa msimu huu tayari Kagere ametupia mabao manne ndani ya Simba huku akizidi kupewa nafasi ya kufanya vizuri licha ya kukwama kuona nyavu kwenye mechi mbili za hivi karibuni.

Kwa sasa kinara wa utupiaji ni John Bocco ambaye amefunga jumla ya mabao 8, huyu pia ni nahodha wa Simba.

Adam Adam ni nyota anayekipiga ndani ya JKT Tanzania ametupia jumla ya mabao 7.

Prince Dube,staa wa Azam FC alianza kwa kasi kabla ya kupata majeraha ambayo yamemuweka nje ya uwanja ametupia jumla ya mabao 6.

Meshack Abraham ni mali ya Gwambina FC kibindoni ametupia jumla ya mabao 6.

Clatous Chama kiungo nyota wa Simba yeye ametupia jumla mabao 6.

KIPA SIMBA AIBUKIA IHEFU FC




DEOGRATIUS Munish maarufu kama Dida sasa atakuwa ni mali ya Ihefu FC inayoshiriki Ligi Kuu Bara kwa msimu wa 2020/21.






Kipa huyo ambaye amewahi kuitumikia Klabu ya Simba msimu wa 2018/19 na kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Bara aliwahi pia kuwa kipa namba moja ndani ya Klabu ya Yanga.




Baada ya kuachwa na Simba alitumika ndani ya Klabu ya Lipuli FC ambayo kwa sasa imeshuka Ligi Kuu Bara na inapambana kurejea ndani ya ligi ikiwa inashiriki Ligi Daraja la Kwanza.




Habari zinaeleza kuwa Dida anaibuka ndani ya Ihefu FC kuongeza nguvu kwenye lango kutokana na timu hiyo kuwa kwenye mwendo wa kusuasua.




Ikiwa imecheza jumla ya mechi 15 imefungwa jumla ya mabao 18 na imefunga mabao 6.




Kocha Mkuu wa Ihefu FC, Zuber Katwila amesema kuwa kwenye dirisha dogo wanahitaji kusajili wachezaji wenye uzoefu ili kuongeza nguvu ndani ya kikosi hicho.

MANARA AFUNGA NDOA, APEWA WOSIA NA KIKWETE




OFISA Habari wa Klabu ya Simba, Haji Manara, usiku wa kuamkia leo Desemba 10, amefunga ndoa na mkewe Naheeda, katika msikiti wa Masjid Maamur.

Ndoa yake imehudhuriwa na watu mbalimbali akiwemo Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Dkt. Jakaya Kikwete, Shehe Mkuu wa mkoa wa Dar, Alhad Mussa Salum na watu wengine wengi maarufu.

Kikwete amesema kuwa Haji alimfuata nyumbani na kumshirikisha jambo hilo kwa ajili ya ndoa na akamuahidi kuja.

Kikwete amesema:"Hakuna ufundi kwenye ndoa kikubwa ni kustahimiliana na kuvumiliana kwa kuwa hakuna ufundi katika ndoa.

"Mnapaswa kuwa makini na kuskilizana katika ndoa, pia nakushauri ujue kwamba uwe na uvumilivu na kuona namna gani mnaweza kuleta watoto kwa kuulizana na kujua mambo yatakuaje.

"Baraka za Mungu kwa watoto ni zake ka kadri atakavyoamua, yale makundi yaache kwa kuwa kila mmoja anajua anachokipenda.




"Nilikuwa ninazungumza na mzee hapo nyuma akaniambia kwamba anahitaji wajukuu hivyo ni jambo la kheri na linahitaji subira kikubwa ninawapongeza katika hilo na ninaamini kwamba itakuwa kheri," amesema.

SVEN VANDENBROEC ATAJA SABABU YA KUMUACHA BONGO MORRISON

 



KOCHA Mkuu wa Simba, Sven Vandenbroeck amesema kuwa nyota wao ambao wamebaki Bongo ni mpango na mbinu ya kiufundi kwa ajili ya mechi zijazo.
Miongoni mwa nyota ambao watakosekana kwenye mchezo wa leo ni Bernard Morrison mwenye bao moja na pasi mbili kiungo mshambuliaji wa Simba atakosekana kwenye mchezo wa Leo Desemba 13 dhidi ya Mbeya City utakaochezwa Uwanja wa Sokoine majira ya saa 10:00 jioni.
Morrison hakusafiri na timu ambayo ilikwea pipa Desemba 11 kuwafuata wapinzani wake ambao watakutana leo Uwanja wa Sokoine.
Mbali na Morrison nyota wengine ni Ibrahim Ajibu mwenye bao moja na pasi mbili za mabao Charles Ilanfya, Kenedy Juma ambao wamepewa program na Sven Vandenbroeck huku Larry Bwalya mwenye pasi moja ya bao yeye ana matatizo ya kifamilia.


Kocha Mkuu wa Simba, Sven Vandenbroeck amesema kuwa sababu ya kuwakosa nyota hao ni kutokana na mpangilio wa ratiba ili wawe bora zaidi.

"Kuna wakati inabidi umpumzishe mchezaji ili awe bora kwenye mechi ijayo au kama sehemu ya mpango wa mbinu na ufundi,".

SIMBA WATANGAZA MCHAKATO WA UCHAGUZI WA MWENYEKITI

 


MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu Bara Klabu ya Simba, leo imetangaza mchakato mzima wa uchaguzi mdogo wa kujaza nafasi ya mwenyekiti utakaoanza leo Desemba 13, na kutarajiwa kukamilika Februari 7, mwakani,

Nafasi hiyo kwa sasa anaikaimu, Mwina Seif Kaduguda baada ya kuachwa wazi na aliyekuwa Mwenyekiti wa Klabu hiyo, Swedi Mkwabi aliyejiuzulu wadhifa huo Septemba 14, mwaka jana baada ya kuhudumu kwa takribani miezi kumi pekee.

Akizungumza na Waandishi wa Habari leo, Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ndani ya klabu hiyo, Boniface Lihamwike amesema: "Tunataka kuwahakikishia Wanasimba na wadau wote wa michezo kiujumla kuwa uchaguzi huu utakuwa huru na wa haki.

Akitoa ratiba ya mchakato huo, Makamu Mwenyekiti wa Kamati, Steven Ally amesema: "Mchakato wa uchaguzi mdogo wa kujaza nafasi ya Mwenyekiti wa Klabu ya Simba umeanza rasmi leo baada ya taarifa hii, na utaendelea mpaka Februari 7, 2021 ambapo ndiyo tunatarajia kufanya uchaguzi na kutangaza mshindi wa nafasi hiyo.

"Kwa taarifa zaidi kuhusu mchakato mzima tumebandika ratiba hii makao makuu ya klabu lakini pia watu wanaweza kuipata kupitia mitandao yetu ya kijamii, vigezo vya kuchukua fomu ni vile ambavyo vimewekwa bayana na Ibara ya 27 ya katiba ya klabu na pia vinapatikana kwenye fomu.

"Lakini kwa uchache ni lazima mgombea awe na elimu ya angalau Shahada inayotambuliwa na tume ya vyuo vikuu Tanzania (TCU), na kadi ya mwanachama hai kwa miaka mitatu huku gharama kwa fomu ikiwa ni Shilingi laki tatu," .

SIMBA YALIA NA WAAMUZI BONGO

 


LICHA ya Simba kuibuka na ushindi wa bao 1-0 jana Desemba 13 na kusepa na pointi tatu mazima mbele ya Mbeya City, uongozi umeshusha lawma kwa waamuzi.

Bao la ushindi kwa Simba lilipatikana kipindi cha Kwanza kupitia kwa nahodha John Bocco aliyepachika bao hilo kwa pasi ya Clatous Chama. 

Mwamuzi wa kati jana alikuwa ni Martin Sanya alijitahidi kwenda na presha ya mchezo wa jana kutokana na timu zote kuwa na uhitaji wa pointi tatu. 


Mbeya City malengo yao makubwa ni kujinasua kwenye mstari wa kushuka daraja na Simba wao jambo lao ni kutetea ubingwa wa Ligi Kuu Bara. 


Mtendaji Mkuu wa Simba, (CEO), Barbara Gonzalez amesema kuwa bado maamuzi ya waamuzi ni tatizo ndani ya Ligi Kuu Bara. 


Ushindi wa Simba jana unaipandisha kutoka nafasi ya tatu mpaka nafasi ya pili ikiwa na pointi 29 baada ya kucheza mechi 13.


Yanga ni vinara wakiwa na pointi 37 baada ya kucheza mechi 15 na nafasi ya tatu ni Azam FC wenye pointi 27 baada ya kucheza mechi 14.


Mbeya City ipo nafasi ya 16 baada ya kucheza mechi 15 na ina pointi 12 kibindoni. 

BEKI SIMBA ATAJWA NDANI YA COASTAL UNION

 



IMEELEZWA kuwa beki wa kati wa Yusuph Mlipili ameingia anga za Coastal Union inayonolewa na Kocha Mkuu,  Juma Mgunda. 


Mlipili ambaye aliachwa na Simba msimu uliopita kutokana na kukosa nafasi kikosi cha Kwanza ni miongoni mwa wazawa mwenye uwezo mkubwa akiwa ndani ya uwanja.


Ujio wa Joash Onyango na Pascal Wawa ambao ni mabeki wa kati uliongeza ufinyu wa namba kikosi cha Kwanza jambo lililofanya nyota huyo apigwa chini mazima licha ya uwezo wake.


 Mgunda ameweka wazi kwamba moja ya sehemu ambayo ataifanyia maboresho ni sehemu ya beki kwa kuwa baada ya kuondoka kwa pacha ya Bakari Mwamnyeto anayekipiga Yanga na Ibrahim Ame ndani ya Simba mambo yamekuwa magumu.


Kwa msimu wa 2020/21 inashikilia rekodi ya kufungwa mabao mengi ambayo ni 7-0 ilifungwa na Simba, Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Arusha.


Mgunda amesema:"Ni lazima nifanyie maboresho safu yangu ya ulinzi na ushambuliaji Kwenye dirisha dogo hivyo mipango ikikamilika kila kitu kitawekwa wazi,".

Kagere bado yupoyupo sana Simba






MSHAMBULIAJI wa Simba, Mnyarwanda Meddie Kagere ni miongoni mwa nyota ambao huenda wataanza kutambulishwa wakati wowote kuanzia leo Jumanne kama alivyoahidi na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Simba, Mohamed Dewji juzi Jumapili alipozungumza na Waandishi wa Habari.


Kagere ambaye ni Mfungaji Bora wa Ligi Kuu Bara kwa misimu miwili mfululizo, kwasasa yupo nchini kwao Rwanda akiitumikia timu yake ya taifa ya Amavubi katika mechi za kuwania kufuzu kwa fainali za Mataifa ya Afrika (AFCON), ingawa viongozi wa Simba walidai kuwa ni kujiweka sawa kwa mazoezi mepesi.


Kagere aliondoka nchini huku akiacha maswali kwa mashabiki wa Simba kwani aliumia mazoezini wakijiandaa kucheza na Prisons hivyo viongozi walidai walimruhusu kwenda kwao kwa ajili ya matibabu zaidi.


Kumekuwapo na taarifa za kwamba Kagere hataendelea na mabingwa hao watetezi wa Ligi Kuu Bara mara mkataba wake wa awali utakapomalizika mwishoni mwa msimu huu kutokana na kukosa nafasi ya kucheza mara kwa mara katika kikosi cha kwanza lakini Mo Dewji alisema hilo litajulikana kuanzia leo Jumanne pamoja na nyota wengine.


Habari za ndani kutoka Simba zinaeleza kwamba straika huyo tayari ameongeza mkataba mpya kuitumikia Simba hivyo atakuwa ni miongoni mwa wale watakaoanza kutangazwa kwenye mitandao ya Simba kuanzia leo Jumanne saa 7 mchana kama bosi huyo alivyosema.


“Kagere alisaini mkataba, pengine ndiye atakayeanza kutambulishwa kama bosi alivyosema, maana kila kitu alisimamia mwenyewe, wapo wengine ambao ni muhimu na mikataba yao ilikuwa inaelekea mwishoni nao wameongeza aliyekuwa amebaki ni Chama (Clatous).

SIMBA YATOSHANA NGUVU NA AFRICAN SPORTS



KIKOSI cha Simba leo kimalazimisha sare ya bila kufungana na timu ya African Sports kwenye mchezo wa kirafiki uliochezwa Uwanja wa Azam Complex.

Chini ya Kocha Mkuu, Sven Vandenbroeck leo langoni alikaa kipa namba tatu, Ally Salim na kuliweka lango lake salama ndani ya dakika 90.

Kwa upande wa safu ya ushambuliaji chini ya nyota Charlse Ilanfya imeshindwa kufurukuta kupata bao mbele ya Klabu ya African Sports.

Sven amefanya mabadiliko makubwa kwenye kikosi cha leo ambapo amewatumia vijana wengi chini ya miaka 20 ili kuwapa uzoefu.

Miongoni mwa nyota hao ni pamoja na Hassan Mohamed,Omary Kazi, Isack Mohamed, Godfrey Mbomahenga, Seif Suleman na Hamis Manguka.

Wale wa kikosi cha kwanza ilikuwa ni pamoja na kiungo Clatous Chama,Francis Kahata, Ibrahim Ame, Kened Juma, Miraj Athuman, Rarry Bwalya na Beno Kakolanya.

MSHAMBULIAJI SIMBA AAHIDI KUFUNGA MABAO MENGI AKIPEWA NAFASI NA SVEN




MSHAMBULIAJI wa Klabu ya Simba, Charlse Ilanfya amesema kuwa ikiwa Kocha Mkuu wa timu, Sven Vandenbroeck atampa nafasi ya kuanza kwenye kikosi cha kwanza atafunga mabao mengi.

Ilanfya ameibukia ndani ya Simba akitokea Klabu ya KMC ambapo akiwa huko msimu wa 2019/20 aliweza kutupia mabao sita na kutoa jumla ya pasi tatu za mabao.

Maisha yake ndani ya Simba yamekutana na ushkaji na benchi kutokana na ushindani wa namba hasa kwa nafasi ambayo anacheza sambamba na nahodha John Bocco mwenye mabao manne sawa na Meddie Kagere.

Simba ikiwa imecheza mechi 10 za ligi ameanza kikosi cha kwanza mchezo mmoja na hakumaliza dakika 90 ilikuwa Uwanja wa Nelson Mandela wakati Simba ikionja joto ya kuyeyusha pointi tatu kwa kufungwa bao 1-0.

Nyota huyo amesema:"Ikiwa kocha atanipa nafasi ya kuanza kikosi cha kwanza mara kwa mara ninaamini kwamba nitafunga mabao mengi kwa timu yangu.


"Kila mchezaji ni bora nami ninapambana kuwa bora na nikipata nafasi nitaonyesha uwezo wangu wa kufunga kwani hiyo ni kazi yangu."

Kwenye msimamo Simba ipo nafasi ya tatu ikiwa na pointi 20 baada ya kucheza mechi 10 na namba moja ni Azam FC mwenye pointi 25 na ile ya pili ipo mikononi mwa Yanga wenye pointi 24.

MO AJA NA MKAKATI KWA AJILI YA SIMBA QUEENS

MO AJA NA MKAKATI KWA AJILI YA SIMBA QUEENS



MWENYEKITI wa Bodi ya Wakurugenzi wa klabu ya Simba, Mohamed Dewji (Mo) amefunguka kuwa, katika vipaumbele ambavyo wametaka kuvifanyia kazi ni pamoja na kuboresha maslahi ya timu ya Simba Queens pamoja na benchi la ufundi.


Mo alisema licha ya kuwa timu hiyo ilitwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Wanawake msimu uliopita imekuwa haipati kile inachostahili kutokana na wachezaji wa timu hiyo kutokuwa na mikataba rasmi ya kufanya kazi ndani ya klabu hiyo.

Mo aliyasema hayo wikiendi iliyopita alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari za michezo kwenye ukumbi wa mikutano uliopo kwenye ofisi yake Posta jijini Dar es Salaam ambapo aliweka wazi kuwa wao kama viongozi wana mipango endelevu na ya muda mrefu kwa timu hiyo.

"Tunahitaji kuboresha maisha, maslahi ya Simba Queens kwa maana ya wachezaji na benchi la ufundi. Unajua hawa wachezaji licha ya msimu uliopita kuwa mabingwa walikuwa hawapati wanachostahili kutokana na ukweli kwamba wengi hawana mikataba rasmi.

"Kwahiyo tumeanza kwanza na wachezaji ambao watakuwa wanahitajika na benchi la ufundi kwa ajili ya msimu ujao. Hii timu tuna mipango nayo ya muda mrefu na tunaipenda sana," amesema Mo.

CHAMA CLATOUS AFUNGUKIA ISHU YAKE YA KUIBUKIA YANGA


 CLATOUS Chama, nyota wa Klabu ya Simba ameweka bayana mpango wake wa sasa ni kuitumikia timu hiyo na hana mpango wa kuibukia ndani ya Yanga.

Hivi karibuni habari zimekuwa zikieleza kuwa Yanga ipo kwenye mpango wa kuinasa saini ya nyota huyo raia wa Zambia ambaye ana tuzo ya mchezaji bora kwa msimu wa 2019/20 baada ya kutoa jumla ya pasi 10 na kufunga mabao mawili kati ya 78 yalifungwa na Simba.

Kwa sasa Chama mwenye pasi tano na mabao mawili kati ya 22 yaliyofungwa na Simba yupo zake nchini Zambia na timu ya Taifa ambayo jana Novemba 12 ilishinda mabao 2-1 dhidi ya Botswana kwenye mchezo wa kufuzu Afcon.

Chama amesema:"Mimi ni mchezaji wa Simba kwa sasa sina mpango wa kwenda Yanga mjomba, bado nitakuwa ndani ya Simba ikitokea kutakuwa na mabadiliko yoyote kila kitu kitakuwa wazi," .

Desemba 15 dirisha dogo la usajili linatarajiwa kufunguliwa Bongo ambapo jina ambalo limekuwa gumzo kwa sasa ni nyota huyo ambaye wengi hupenda kumuita mwamba wa Lusaka.

Habari kutoka ndani ya Simba zinaeleza kuwa tayari wamemuongezea mkataba wa miaka miwili utakaomfanya abaki ndani ya timu hiyo yenye ngome yake Msimbazi.

KOCHA SIMBA AUFIKIRIA MUZIKI WA PLATEAU YA NIGERIA

 KOCHA Mkuu wa Simba, Sven Vandenbroeck amesema kuwa hesabu kubwa kwa sasa ndani ya kikosi hicho ni kwenye mchezo wao wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Plateau United ambayo ni imara kwenye safu ya ushambuliaji.

Simba ina kazi ya kuanza kusaka ushindi kwenye mchezo wa kwanza ugenini nchini Nigeria mchezo unaotarajiwa kuchezwa kati ya Novemba 27-29, mchezo wa marudio unatarajiwa kuchezwa Desemba 4-6.

Sven amesema kuwa wanakutana na timu bora hasa kwenye safu ya ushambuliaji jambo ambalo linawafanya waichukulie kwa uzito mkubwa mechi hiyo.

Kocha huyo raia wa Ubelgiji amesema:”Ukiwa unakutana na mpinzani ambaye ni mzuri kwenye safu ya ushambuliaji hapo ni muhimu kuongeza nguvu hasa kwenye ulinzi ili kutoruhusu kufungwa, ninawajua wapinzani wetu hiyo tutajipanga kufanya vizuri,” amesema.


Popular Posts